Google PlusRSS FeedEmail

BIEBER AKATISHA SHOO JUKWAANI BAADA YA KUUGUA GHAFLA




Msanii chipukizi wa miondoko ya Pop kutoka nchini Marekani Justine Bieber ameugua ghafla na kukatisha shoo aliyokuwa akifanya

Tukio hilo lilitokea wakati msanii huyo alipokuwa akiimba moja ya nyimbo zake wakati yupo katikati ya kushusha mistari aliugua ghafla na kulazimika kukatiza shoo hiyo

Bieber alikuwa akiimba kwenye tamasha lililofanyika katika mji wa Glendale, Arizona ambalo lilikuwa kati ya tamasha kubwa lililowahi kutokea nchini Marekani

Kwa mujibu wa msimamizi wa tamasha hilo alisema kuwa msanii huyo aliondoka jukwaani baada ya tukio hilo, lakini alirejea baada ya muda mfupi wa mapumziko

Baada ya kupanda tena jukwaani Bieber aliwauliza mashabiki wake "Je mtanipenda japokuwa nitakuwa nipo katika hali iliyonitokea hivi karibuni juu ya jukwaa?"

Baadae msanii huyo aliandika katika ukurasa wake wa kijamii Twitter kuwa "Maziwa yalikuwa siyo chaguo lake sahihi lo!"

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging