LUTENI KALAMA AJA NA 'KAMA NANI'
Msanii wa kundi la Gangwe Mobb, Luteni Kalama ameibuka kivyake na kibao 'Kama Nani' akimshirikisha msanii chipukizi aitwaye Neighbour wa jijini Dar es Salam
Akizungumza jijini Dar es Salaam juu ya ujio wa kibao hicho ambacho kimetoka sambamba na video yake tayari kimeshaanzwa kusambazwa katika baadhi ya redio na televisheni
"Nimeamua kuachia kibao hiki kwa kumshirikisha dogo chipukizi kabisa kazi hii imeandaliwa pale Natal Record ya jijini na video nimeifanya prime video singo imeanza kupigwa na kuchezwa katika baadhi ya runinga" alisema Kalama