BEYONCE APATA HEKAHEKA
Imekuwa ni wiki ya hekaheka kwa mwanamuziki mwenye makazi yake Texas, Beyonce, akijikuta akidhalilika baada ya kugundulika kuwa hakufanya shoo yake live na badala yake ilikuwa ni rekodedi.
Mashabiki waliohudhuria onyesho hilo walidhani kuwa amefanya shoo hiyo live kabla ya kugundua kuwa shoo hiyo ilikuwa ya kurekodiwa, kitu ambacho kiliwafanya kulalamika
Mwanamuziki Kelly Clarkson aliyepanda kabla ya Beyonce alicheza muziki wake 'Live'
Taarifa hizo zimekuja wakati mbaya kwa Beyonce kwa kuwa mwanamuziki huyo amekuwa katika jitihada la kujiunga tena na kundi la Destiny Child huku kukiwa na tetesi kibao kuhusiana na uhusiano na mume wake pamoja na mtoto wake.








