Google PlusRSS FeedEmail

PRO 24 DJ'S KUFANYA MAKAMUZI TBC ONE USIKU WA VALENTINE



Wakati baadhi ya watu wanafanya tasmini na kufikiria jinsi gani watakavyosherehekea na kuifanya siku ya wapendanao 'Valentine day'iwe ya kipekee na yenye utofauti, Pro 24 Djs kama kawaida wamejipanga kwa ajili ya kufanya shoo ya kipekee 'Crazzy Show' kwenye kipindi cha Bang na Pro 24 siku hiyo ya Alhamisi ambapo ni siku ya wapendanao

Kipindi ambacho kinarushwa kila siku ya alhamisi katika Televisheni Taifa ya (TBC one) kuanzia saa nne mpaka sasa saba usiku ambapo Crazzy Djs wanafanya video mix zenye radha tofauti tofauti ili kuukamilisha usiku wako

Dj Dea ni mmoja wa madj wa pro 24 ambao atafungua kipindi hiko kwa muda wa kwanza huku akipiga nyimbo zenye miondoko na radha tofauti tofauti

Pro 24 wameandaa usiku huo ili kuendelea kutoa burudani kwa mashabiki wake huku wakiwa wanapiga nyimbo yaani video mix tofauti tofauti zinazotamba duniani kote


This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging