Google PlusRSS FeedEmail

BBA THE CHASE: UGANDA OUT, FEZA CHUPUCHUPU.

SAFARI ya mwisho kwa washiriki kutoka Uganda kwenye shindano la Big Brother The Chase ilihitimishwa jana kwa mshiriki aliyebakia LK4 kuyaaga mashindano hayo baada ya kura zake kutotosha kumbakisha. Mshiriki wa kwanza wa Uganda Denzel alitolewa katika wiki ya kwanza pamoja na mshiriki kutoka Kenya Huddah, kwa maana hiyo Uganda kwasasa haina mshiriki hata mmoja aliyebakia kwenye jumba hilo. 
Nchi zingine zilizoko katika hatari ya kukosa washiriki kwenye jumba hilo ni pamoja na Kenya ambayo imebakiwa na mshiriki mmoja ambaye anaitwa Annabel na Afrika Kusini ambayo nayo jana ilipoteza mshiriki mmoja ambaye ni Koketso na kubakiwa na Angelo pekee. 
Kwa upande wa Tanzania mshiriki wetu Feza ambaye alikuwa kikaangoni alipona baada ya kura zake kutosha kumbakisha katika jumba hilo baada ya Betty aliyekuwa HOH kumtoa mpenzi wake Bolt katika kikaango na kumuingiza Feza. Shindano hilo linaendelea kwa washiriki kupendekeza tena washiriki ambao wangependa waingie katika kikaango kabla ya kupigiwa kura na watazamaji mshiriki ambaye wanaona anafaa kubakia ndani ya mjengo huo.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging