Google PlusRSS FeedEmail

H.BABA NA FLORA MVUNGI WAPATA MTOTO WA KIKE, H. BABA AELEZEA UNDANI WA JINA LA MTOTO WAO TANZANITE

HATIMAYE wanandoa wawili ambao ni wasanii wa filamu Flora Mvungi pamoja na msanii wa muziki wa kizazi kipya miondoko ya Bongo Bolingo Fleva Hamis Ramadhan 'H. Baba' wamepata mtoto wa kike na kumpa jina la Tanzanite.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii dhumuni la kumpa jina hilo mtoto huyo, H. Baba aliweka wazi kuwa ameamua kumpa jina hilo mtoto wake ikiwa ni jina la madini yanayopatikana nchini Tanzania tu.

Alisema kuwa madini hayo yanapatikana nchini na ndio yanayotangaza utaifa wa Tanzania hivyo kwa upande wake hajaamua kimakosa kumpa jina mtoto huyo.

"Unajua madini ya Tanzanite ndio pekee yanayoipatikana nchini huwezi ukayapata madini hayo nje ya nchi, ndio maana mtoto wangu nimempa jina hilo nikimfafanisha na madini hayo" alisema H. Baba.

Wasanii hao ambao wamefunga ndoa yao hivi karibuni huyo ndiye mtoto wao wa  kwanza walioamua kumuita jina hilo ambapo wananamfafananisha na madini hayo yanayopatikana nchini.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging