CIARA ABADILI MUONEKANO WA MAVAZI
Msanii wa R&B , kutoka nchini Marekani Ciara mwenye mahusiano na msanii mwenzake Future hivi karibuni ameonekana akiwa na muonekano wa tofauti baada ya kubadilisha mtindo wake wa mavazi huku akihisiwa kuwa ni mjamzito.
Hivi karibuni Ciara alikuwa Airport na alionekana akiwa na mbwa ambaye amembeba huku ikidhaniwa kuwa anaficha tumbo lake, ambapo pia ameonekana kwenye show mbalimbali akiwa amevaa vazi la kuficha tumbo hali ambayo si ya kawaida








