Google PlusRSS FeedEmail

HASHIM KAMBI NA VAN VICKER WACHEZA FILAMU YA PAMOJA

                            Van Vicker, Irene Paul
Ni hali ya kawaida kwa watunzi wa filamu zetu Bongo kuandika sinema kisha baadaye kutafuta jina la sinema hiyo pasipo kufanya utafiti kama jina hilo linaweza kuwa na mwingiliano na filamu nyingine ambayo tayari imetoka au hata kusajili katika taasisi zinazohusika kufanya hivyo, hayo ndiyo yaliyotokea katika filamu ambayo mwigizaji kutoka Ghana Van Vicker ameigiza Bongo.

Mtayarishaji wa filamu hiyo Hashim Kambi ‘Ramsey’ amesema kuwa msanii huyo Van Vicker ambaye alimwalika kuja kushiriki katika filamu yake hiyo ameigiza katika filamu vizuri sana na kuwapa somo wao, lakini hadi anaondoka filamu hiyo ilikosa jina kwa sababu mtunzi wa filamu hiyo Leah Mwendamseke ‘Lamata’ alitaja jina ambalo kuna sinema .

“Unajua nilisoma hadithi yake na kuipenda kwa hiyo alivyokuja Van Vicker tualianza kurekodi Director Simon Mwakifwamba wangu akaliona lile jina na ambalo ni Mtandao na kubaini kuna filamu hiyo, baadaye Lamata akasema iitwe Network kumbe tayari kuna sinema ya MFDI ipo kwa jina hilo,”anasema Ramsey’.

Hadi inamalizika kurekodiwa sinema haikuwa na jina hivyo wanamsubiri Van Vicker awatungie jina kwani wakati akiondoka aliwashauri wasubiri akifika Ghana atangalia jina la kuipa na wao kutumia, changamoto ni kubwa sana hadi jina la filamu linatoka nje wakati watunzi wapo hapa kuna changamoto katika tasnia ya filamu

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging