Google PlusRSS FeedEmail

NANI KAMWAGA POMBE YANGU YAMUINGIZIA MADEE ZAIDI YA MILIONI 32

Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Madee ameweka wazi kuwa nyimbo yake ya 'Nani kamwaga pombe yangu' imemuingizia mtonyo zaidi ya milioni 140.

Akizungumza katika moja ya mahojiano ndani ya radio ya Clouds FM Madee aliweka wazi kuwa hiyo ndiyo nyimbo yake ya kipekee iliyomuingizia hela kwa muda mfupi hali iliyopelekea kubadili aina ya muziki kuacha muziki wa Hip Hop na kuamini kuwa staili anayoifanya sasa ndiyo ipo kwenye biashara.

Msanii huyo ameweza kukusanya mtonyo huo katika shoo mbalimbali ambapo aliweka mchanganuo wa shoo zake kuwa aliweza kupata shoo 8 za fiesta, pia aliweza kuingia mkataba na kampuni za simu ambapo aliweza kukusanya zaidi ya milioni 80 pamoja na kampuni ya Coca Cola.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging