Google PlusRSS FeedEmail

ZITTO AJIBU SALAMU ZA NEY WA MITEGO




HATIMAYE Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe  amjibu msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Ney wa Mitego kuwa alichokiimba juu yake ni moja ya kazi yake ya sanaa

Zitto alimjibu msanii huyo kupitia ukurasa wake wa Twitter juu ya kile alichokiimba kwenye wimbo wake wa Salamu zao. Zitto alidai kuwa alichokiimba msanii huyo ni moja ya kazi ya sanaa hivyo maneno yake anayachukulia kama changamoto.

"Ney amefanya sanaa,  nachukua maneno yake kama changamoto, ni kazi ya Sanaa ninayoithamini sana" hayo ndio maneno yaliyoandikwa na Zitto kwenye ukurasa wake huo wa Twitter.

Ney wa Mitego hivi karibuni ametoa wimbo unaokwenda kwa jina la Salaamu Zao ambapo moja ya mashairi yake yalimtaka Zitto kuachana na masuala ya Bongo Fleva kwani teyari ameshalitelekeza kundi la Kigoma All Stars.



This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging