Google PlusRSS FeedEmail

TUNAJILINGANISHA NA KANUMBA KWA KIPI NYWELE ZA KISOMALI?

                                                
Watu wengi wamesema wanaomba tufanye reviews za matukio mbalimbali ya sinema na filamu zenyewe kwa ujumla, hivyo tumeweka utaratibu kwa wanataaluma kupitia na kuchambua matukio hayo na kwa kuanza tunaanza na hili la wale wanaojiita akina Kanumba eti wamefanana naye!

               PhilemonLutwaza
    Philemon LutwazaUncle D1 kidogo anamuonekano kama Kanumba: picha kwa hisani ya Global       Publishers.
                Ramy Galis
                                                          Huyu naye wanasema kafanana naye mmmh,,,
                Eliya Daniel
                    Elly G kijana ambaye yeye toka enzi za uhai wa Kanumba alipenda kujifanananisha naye.

Kuna Wakati badala ya kuona aibu wao tunajikuta sisi ndiyo tunaona aibu, unamkuta msanii anahojiwa na Televisheni au Redio kuhusu yeye lakini bila ya uoga wala aibu utasikia ‘Nimefanana sana na marehemu Kanumba, na kila mtu ananisifia’ kauli kama hizi ni kauli za kinyonge, za kijinga zinazorudisha tasnia ya filamu nyuma badala ya kusonga mbele.

Wengi wanajiuliza hao ambao wamefanya mtaji kwa kujifananisha na marehemu Kanumba wanafaidika na nini kwa kujifananisha naye au ni njia ya biashara kwao ambayo siku yoyote inaweza kufa na kupotea kabisa, au bila kutaka jina la msanii nyota hawana jipya wala maarifa ya kutoka?

Hauwezi kuvaa viatu vya mtu bila kumjua vema, wengi ambao wanajaribu kujifananisha na Legend Kanumba walimjua tu kwa sababu alikuwa ni msanii mkubwa na nyota lakini hakuna hata mmoja aliyemsoma na kumfahamu kama ni mtu wa watu na aliweza kuishi na wanahabari pamoja na wapenzi wa filamu kwa ukaribu ikiwa kujitokeza kwao katika mambo yao.

                 Rammy Galis ''Snitch'' 538
                                    Hizi ni sehemu ya kazi zao ambazo zinawafanya watamani kuwa kama Kanumba
                   After death

STORY NA PICHA KWA HISANI YA FC

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging