

“Wapo wengi ambao najua watu watasema kuwa wacheza mpira ni mabwana zangu lakini hakuna ninayetoka naye kimapenzi, mimi sitoki na Mrisho Ngasa lakini nimefanya naye kazi ya filamu yangu ya Majanga sasa watu wanatangaza kama Ngasa ni mtu wangu na natoka naye lakini Ngasa ni msanii tu aliyeshiriki katika filamu yangu,”anasema Snura.

Snura anadai kuwa katika filamu yake ya Majanga Mrisho Ngasa kaigiza kama mmewe au mchamba wake, hivyo iwe kwa bahati mbaya au kuna mtu ambaye aliwaona katika baadhi ya picha na kutangaza kuwa ni wapenzi amekosea msanii huyo anasisitiza kuwa Mrisho amemwigiza katika fani ya uigizaji ni rafiki wa kikazi tu na si vinginevyo.

Msanii huyo ambaye anafanya vizuri katika filamu na muziki hivi sasa nyota yake imeng’ara katika muziki na anatamba na kibao ‘Nimevurugwa’ huku kibao cha Majanga kukiendeleza kwa kukitungia filamu iliyoshirikisha watu maarufu kama akina Mrisho Ngasa ambaye inasemekana anatoka naye naye anasema ni filamu tu...
KWA HISANI YA FC..







