JAY Z 'AMKACHA' KANYE WEST
Habari zilizozagaa kwenye mitandao mbalimbali nchini Marekani zinazodai kuwa msanii wa Hip Hop nchini humo Jay Z kukataa kuwa 'Best Man' msimamizi wa ndoa ya rafiki yake mkubwa Kanye West katika harusi hiyo ambayo inatarajia kufanyika hivi karibuni.
Taarifa hizo zinadai kuwa sababu zilizopelekea msanii huyo kukataa kumsimamia harusi rafikia yake huyo ni kwa madai kuwa Jay Z hapende kutokea katika Reality Tv Show.
Kwa mujibu wa Gazeti la Daily Star limeandika kuwa Jay Z ndio msanii ambaye pia ni rafiki zaidi wa Kanye West na anavigezo vyote kuwa msimamizi wake,
Gazeti hilo liliandika kuwa Jay Z atakubali kuwa Best men wa Kanye West kama hapatakuwa
na mpiga picha wa kipindi hicho cha Kim K.








