Google PlusRSS FeedEmail

MZEE CHILO ATOA SOMO KWA WASANII WENZAKE

Mkongwe katika tasnia ya filamu Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’ amewaasa wasanii wenzake badala ya kulalamikia maamuzi yanayotolewa na Bodi ya Ukaguzi wa Filamu na Michezo ya kuigiza, Mzee Chilo anasema kuwa wasanii na watayarishaji wamekuwa wakilalamikia ukaguzi bila sababu ya msingi huku wakikiuka sheria za nchi zinazofuatwa na bodi hiyo.

“Tuache kulalamika wakati tunavunja sheria zilizowekwa na zipo katika Katiba yetu ya Tanzania, haiwezekani kila mtu akafanya anavyotaka mwenyewe wakati kuna vitu vinaenda tofauti, kila jambo lina utaratibu wake wa kufuatwa ili mila, Desturi zilindwe, hivyo tuiache Bodi ifanye kazi yake,”anasema Mzee Chilo.
          
Mzee Chilo alisema hayo wakati akichangia katika mjadala uliandaliwa na Serikali wakitathimini hali ya soko kwa sasa Tanzania, amesema kuwa wasanii na watayarishaji wawe makini kwa kusoma kanuni na sheria yenyewe ya filamu inasemaje kabla ya kwenda location na kutengeneza sinema ambayo ikija kukaguliwa inakosa sifa za kuingia sokoni na badala yake watu wanaanza kulaumu bodi wakati hawakufuata taratibu.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging