Google PlusRSS FeedEmail

MZEE GURUMO AFARIKI DUNIA

                                         
Mwanamuziki wa bendi ya Msindo Ngoma  Tanzania Mzee Muhidini Maalim Gurumo amefariki Dunia April 13 mchana  katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili

Taarifa zilizothibitishwa na hospitali ya Taifa Muhimbili  zimesema Mzee huyu amefariki Dunia akiwa hospitalini hapo  saa nane mchana baada ya kufikishwa Hospitalini hapo April 12 asubuhi na kulazwa kwenye wodi namba 6 ya Mwaisela kutokana na kuzidiwa.
 

Tayari mwili wake umepelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti ambapo mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu April 14 huko Masaki Kisarawe Katika kijiji alichozaliwa.

Pro24 inatoa pole kwa familia ya mzee Gurumo na wapenzi wa Bendi yake Msondo Ngoma,Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pepa peponi Amina

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging