Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Godfrey Tumaini ''Dudu Baya'' amesema anatarajia kuja kivingine na wimbo wake mpya wa shetani.wimbo huo ambao tayari umeshaanza kusikika katika baadhi ya vituo vya Radio hapa Nchini
Dudu baya amesema wimbo huo unazungumzia mambo mengi katika Jamiii hii Tanzania.
Ameongeza kuwa katika wimbo huo amekemea vitu vingi viovu hasa vinavyofanywa na viongozi wa dini kama Mapadri,wachungaji ,maaskofu ,mashehe na watawa..
Aliongeza kuwa kwa sasa amepania kuja kivingine ili kukonga nyoyo za mashabiki wa muziki wake
Tayari wimbo huo umeshaanza kuasikika katika baadhi ya vituo vya Radio hapa nchini