Google PlusRSS FeedEmail

JESHI LA POLISI LATHIBITISHA KUPOKEA TUHUMA ZA UBAKAJI MUMEWAKE FLORA MBASHA

BAADA ya habari kusambaa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, juu ya tuhuma za mume wa muimbaji wa nyimbo za Injiri Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha hatimaye jeshi la Polisi limethibisha kupokea tuhuma za ubakaji dhidi ya mume wa mwimbaji wa injili Flora Mbasha anayefahamika kwa jina la Emmanuel Mbasha.

Akidhibitisha juu ya kutokea kwa tukio hilo, kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi wa Ilala, Marietha Minangi ameeleza kuwa jeshi hilo limepokea tuhuma hizo kutoka kwa mlalamikaji ambaye ni binti mwenye umri wa miaka 17 na kwamba binti huyo alifika katika kituo cha polisi akiwa na ndugu zake.

“Taarifa zimepokelewa na zinachunguzwa. Taarifa zilizokuja ni za kubaka sasa tunazichunguza tufike mwisho tujue ni nini.”alisema  Kamanda Minangi

Ameeleza kuwa baada ya kupata taarifa hizo kutoka kwa mlalamikaji polisi walienda nyumbani kwake ambapo hawakumkuta yeye na mkewe na kwamba hadi sasa hawajapatikana.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging