Timu ya kipindi cha mboni show imepata ajali mbaya ya gari,mara baada ya gari waliokuwa wakisafiria kupasuka tairi,
Marehemu Geogre Tyson pichani hapa alikuwa yupo kijiji cha Chilonwa Chamwino kwenye utoaji wa madawati katika shule ya msingi Chaula iliyopo Dodoma. Baada ya kumaliza shughuli hii huku akiwa kama producer wa The Mboni Show mauti yalimkuta majira ya saa 12 jioni akiwa njiani kurudi Dar es Salaam
Katika gari hilo walikuwa watu 8 ila yeye pekee ndio aliyepoteza mauti na wengine kupata majeraha mwilini pamoja na dereva wa gari hilo. Kwa sasa mwili wa marehemu uko njiani kuletwa jijini dar es salaam kusubiri ratiba ya mazishi.
Mwenyezi Mungu Ailaze roho ya marehemu Geogre Tyson mahala pema peponi.Amin
Baadhi ya picha zikionyesha gari walilokuwa wakisafiria marehemu na wenzake
Msanii wa Bongo Fleva AY akiwa amewasili na kumpa pole Mboni Masimba, AY aliweza kununua jeneza la marehemu Tyson ili kuweza kuusafirisha mwili mpaka Hospital ya Kairuki iliyopo Mikocheni Jijini Dar es salaam
PICHA KWA HISANI YA DJ CHOKA