WANAMUZIKI kutoka nchini Marekani, Jay Z na Beyonce wameamua kubadilisha mtindo wa nywele za mtoto wao Blue Ivy ikiwa ni siku chache baada ya watu kuanzisha kampeni ya kuwashinikiza kumchana nywele mtoto wao.
Kampeni hiyo iliibuma mara baada ya wazazi hao wawili kuonekana kutojali nywele za mtoto wao huo ambapo hata kuchanwa ilionekana ni jambo ambalo haliwezekani.
Wasanii hao wameonekana wakiwa kwenye yatch na mtoto wao huko Miami wakati wanaendelea na ‘On The Run Tour’ na wakiwa na furaha huku nywele za mtoto wao zikiwa kivingine.
Haijaeleweka kama zoezi hilo ndio chanzo cha wao kubadili mtindo wa nywele za Blue Ivy ama ni mpango wa maisha yao tu ya kawaida.
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.