Google PlusRSS FeedEmail

MADAKTARI WAPUNGUZA UUME WAKE, AACHWA NA MKE WAKE



Madaktari nchini Canada wameingia katika matatizo makubwa baada ya kukosea na kumkata mwanaume mmoja sehemu ya uume wake na kupunguza kwa urefu wa inch 1 (sentimeta 2.5).

Kwa mujibu wa QMI la Canada, mwanaume huyo anadaiwa kufika hospitali akihitaji matibabu baada ya kuumia bahati mbaya wakati wa tendo la ndoa na kupata mshituko hivyo kulazimika kufanyiwa upasuaji ili kumsaidia kuituliza mishipa iliyokuwa hatarini.

Lakini baada ya kumaliza tiba aligundua kuwa amekatwa sehemu ya uume wake na madaktari wakadai ilikuwa bahati mbaya.

Kufuatia tukio hilo, anadai alishindwa kufanya mapenzi kwa muda wa miaka miwili hivyo mke wake ambaye jina lake halikutajwa na vyombo vya habari vya Canada, aliamua kuachana nae.

Uamuzi wa mwanamke huyo ulimvuruga zaidi mwanaume huyo ambaye ameamua kufungua mashitaka dhidi ya madaktari waliomfanyia upasuaji.

Mwanaume huyo anadai fidia ya $155, 000 kwa uzembe uliofanywa na madaktari hao kwa kuwa inaelezwa hawakufuata taratibu zote za awali kabla ya kumfanyia upasuaji.

“Hii imenifanyia madhara makubwa katika maisha yangu zaidi ya siku niliyoumia miguu yangu na kushindwa kutembea.”

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging