Google PlusRSS FeedEmail

NICKI MINAJ ANANINI NA IGGY AZALEA?

Rapper wa kike raia wa Australia, Iggy Azalea amezungumzia taarifa zilizoenea kwenye vyombo vya habari kuwa Nicki Minaj alimdiss wakati anatoa hutuba baada ya kupokea tuzo ya rapper bora wa kike kwenye BET Awards, June 29.

Iggy Azalea ameandika kwenye Instagram ujumbe mrefu kuhusu taarifa hizo na kueleza kuwa taarifa hizo hazimsumbui hata kidogo na kwamba amechoshwa na watu wanaojaribu kumsukuma kwenye vita na wasanii wenzake.

“Kwa kuzumza kwa ujumla, sijasumbuliwa na chochote kilichotokea kwenye tuzo za BET na najihisi kutahadharishwa na yeyote anateka kunifanya niwe na vita na watu muda woe. Nachukia kona kila mmoja anakasirishwa kwa niaba yangu kaika vitu ambavyo sijawa na uhakika navyo 100% kama vipo na havijalishi. Nikuacha tu vipite.” Iggy aliandika kwa lugha ya kiingereza.

Taarifa za first lady wa Young Money kudaiwa kumdiss Iggy zilitokana na maelezo ya Nicki Minaj baada ya kupokea tuzo yake ambapo alidai kuwa anachotaka dunia ifahamu kuhusu yeye ni kwamba wanapomsikia Nicki Minaj anarap waelewe kwa yeey ndiye aliyeandika.

Hiyo iliunganishwa na kile kinachodaiwa kuwa Iggy Azalea huwa anawatumi watu mbalimbali kumuandikia mashairi ya nyimbo zake.

Hata hivyo, Nicki Minaj alikanusha kumdiss rapper huyo wa kike kupitia tweets zake na kuvirushia lawama vyombo vya habari.

“The media puts words in my mouth all the time and this is no different. I will always take a stance on women writing b/c I believe in us! I believe we're smart enough to write down our own thoughts and perspective, just like the men do. I've been saying this for 5 YEARS.”

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging