bn
MSANII mkongwe wa filamu Bongo Blandina Chagula ‘Johari’ ametamba kuwa amelinda muonekano wake na kuonekana bado kijana tofauti na wasanii wa kike wengine ambao wanaonekana umri umeenda japo ni wasichana wadogo, lakini wanaonekana akina mama watu wazima.
Akitolea mfano alisema kuwa msanii kama Irene Uwoya anaonekana mkubwa kwake lakini ni mdogo wake mbali, Johari anasema kuwa alikuwa ameamua kuwa mtayarishaji tu, lakini anarudi tena kama mwigizaji baada ya kuona wasanii wengi viwango vyao ni vya kawaida sana katika uigizaji.