Google PlusRSS FeedEmail
Showing posts with label MOVIES. Show all posts
Showing posts with label MOVIES. Show all posts




Msanii Elizabeth Michael aka Lulu leo ametambulisha Filamu yake Mpya ambayo imeingia sokoni leo iitwayo MAPENZI YA MUNGU, huku akiwa amemshirikisha Msanii wa Bongo Fleva Linah Sanga na Mama Kanumba.

Wakati akiilezea filamu hiyo mbele ya wanahabari Lulu amesema Kuwa Ni Filamu inayofundisha na Kutoa somo kwa mtu yoyote yule ambae yupo hapa Duniani kwa kuendelea kuonyesha kuwa MUNGU YUPO. Akiongezea kuwa..."Sisi kama binadamu tumekuwa tukifanya mambo mengi sana hapa Duniani na kupelekea kumsahau Mungu na pengine kuendelea kufikiria kuwa yote tuyafanyayo ni kwa uwezo wetu kumbe Sio uwezo wetu na Ni Mapenzi ya Mungu tu ndio yanayofanya sisi kufikia hapa tulipo leo"

Filamu ya MAPENZI YA MUNGU imekuwa gumzo kabla ya kutoka kutokana na watanzania wengi kuwa na shauku ya Kutaka kumuona Lulu tena mara baada ya Kuonekana katika Filamu Zake Mbili zilizotangulia za FOOLISH AGE na FAMILY CURSE. Sasa Lulu kuonekana tena katika kiwango cha Juu katika Filamu hii Mpya ambayo imeingia Sokoni Leo.

MSANII LULU AITAMBULISHA FILAMU YAKE MPYA IITWAYO MAPENZI YA MUNGU

Msanii Elizabeth Michael aka Lulu leo ametambulisha Filamu yake Mpya ambayo imeingia sokoni leo iitwayo MAPENZI YA MUNGU, huku akiwa ... [Read More]

JACQUELINE WOLPER AMKANA NEY WA MITEGO

                Jackline Wolper amefunguka kuhusiana na moja ya shutuma zinazoendelea kumkabili kila anapoamka. Mdada huyo mwenye kujitu... [Read More]

MERCY JOHNSON AZIDI KUSHIKA KASI

                            Mcheza filamu Mercy Johnson anasadikiwa ndeye msanii tajiri zaidi kuliko wasanii wote wa kike Nchini... [Read More]

NIVA ACHEZEA KICHAPO KUTOKA KWA DEMU WAKE

                                          Mcheza  filamu Zuberi Mohamed‘Niva’ juzi alijikuta akipata fedhea baada ya kupigana na mtu inay... [Read More]

VAN VICKER KUJA NA FILAMU YA UTUMWA

Mshindi wa Tunzo ya filamu ya Pan African Van Vicker anasema kuwa wakati umefika wa kufanya filamu za Historia ya kweli ambayo  haisemwi s... [Read More]

SUSAN PETER NAYE ATAMANI KUIMBA

                                                  Mmoja kati ya waigizaji wenye majina makubwa  nchini Nigeria Susan Peters ameeleza azma... [Read More]

YVONNE : AZIDI KUMTENGA IYANYA KATIKA KAZI ZAKE

                               Katika kuonesha kwamba hapendezwi  kabisa kuwa karibu na aliyekuwa mpenzi wake.Yvone  Nelson amesema kwamb... [Read More]

WAHARAMIA WA KAZI ZA WASANII WABUNI STYLE MPYA

                                          Jeshi la Polisi mkoani Tanga, limefanikiwa kukamata nakala 400 feki za filamu ya Ngema, mali y... [Read More]

Msanii wa filamu wa kike Rachel Haule ameamua kuachana na filamu za kushirikishwa na badala yake kuamua kuwa mtayarishaji wa filamu ambazo pia ataendelea kuigiza katika filamu hizo atakazokuwa akizitayarisha na katika kuhakikisha hilo tayari ameanza na filamu inayokwenda kwa jina la Vanessa in Dillema“Katika tasnia ya filamu Bongo hauwezi kutoka kwa kuigiza filamu za watayarishaji wengine pekee ili uweze kujiongezea kipato lazima uwe na filamu yako hiyo ndio chachu ya kila msanii anajikuta akiamua kutengeneza filamu zake kwa ajili ya kumudu maisha,”anasema Rachel.

Pamoja na kuamua kujitegemea kuandaa kazi zake lakini msanii huyo anadai kuwa kuna Changamoto nyingi ikiwa masuala ya mtaji wa kuweza kutengeneza filamu bora, huku soko nalo likiwa ni tatizo kubwa kwani hakuna wasambazaji wengi hali inayosababisha wasanii kukaa na kazi kwa muda mrefu mkononi bila kuuzwa na kuwafikia watazamaji kwa wakati muafaka

RACHEL HAULE KIVYAKEVYAKE NA VANESSA IN DILLEMA

Msanii wa filamu wa kike Rachel Haule ameamua kuachana na filamu za kushirikishwa na badala yake kuamua kuwa mtayarishaji wa filamu amba... [Read More]



Baada ya story ya mwanadada Jacqueline wolper kutolewa nje pamoja na vitu vyake kuzagaa kwenye vyombo vya habari hususani magazeti, tuliamua kumtafuta mwanadada huyu ili tupate ukweli wa jambo hilo na kuamua kumtafuta hewani

Jacqueline Wolper: Mwanzo nilikuwa nakaa ,Mbezi beach, kwenye apartment ya kama USD 1500 kwa mwezi, na nilikuwa nakaa mwenyewe, na kama unavyojua huwa nawalea wadogo zangu na muda huo walikuwa wapo chuo, Ila walipomaliza nikaona badala ya mimi kukaa mwenyewe ni bora nitafute nyumba nyingine mbili ili wakae wenyewe na mimi nikae mwenyewe. Ndo maana nikahama huko mbezi beach. Sa sijui hao wanaosema nimetolewa vitu nje wanatoa wapi hayo maneno. Labda kama walipiga picha wakati nahama na kuamua kujitengenezea stori.

Unahisi ni kwanini wameandika kuwa umetolewa vitu nje?

Jacqueline Wolper: Mmmh! Siwezi kujua na wala hainisadii, maana sio kweli. Mi sukuona sababu ya kulipa hizo hela kwa mwezi wakati naweza kukaa kwenye nyumba nzuri ya $800 au mia $900 kwa mwezi na nikawatafutia wadogo wangu nyumba nao wakae kwa gharama hiyo hiyo na kwa uhuru wao. Kwangu mimi haina maana hata kidogo kwa sasa kulipa hela zote bila sababu, Wakati nipo mwenyewe ilikuwa sawa ila sasa it doesn’t make sense at all. Kuna mambo mengine ya muhimu ya kufanya. Na isitoshe suala la foleni. So sijui waliondika hivyo wanatafuta nini kwangu.
(Chini ni baadhi ya Picha za nyumba anayoishi jackline wolper sasa baada ya kuhama mbezi)
wp3
wp1

HIKI NDICHO ALICHOSEMA JACKLINE WOLPER BAADA YA MAGAZETI KUANDIKA KUWA AMETUPIWA ZAGA ZAKE NJE YA NYUMBA ALIYOKUWA AKIISHI

Baada ya story ya mwanadada Jacqueline wolper kutolewa nje pamoja na vitu vyake kuzagaa kwenye vyombo vya habari hususani magazeti, tul... [Read More]

Muigizaji Jacqueline “Jackie” Wolper amewashangaa wanaodhani kuwa urembo wa mwanamke ni mbadala wa kipaji hasa katika sanaa ya maigizo.Alisema urembo ni moja ya sifa ya mwanamke lakini kamwe hauwezi kumfanya asiye na kipaji kuwa nacho.“Ukiwa mrembo ni bora zaidi,kwa kuwa itamfanya avutie kwenye movie,lakini pamoja na hayo ni lazima awe na uwezo wa kuigiza kulingana na kipande husika”alisema Wolper.
Wolper aliendelea kulalama kuwa kila mtu akijona ana sura ya kuvutia na umbo zuri basi anajua anaweza kuigiza ndio maana matokeo yake wanafanya vitu sivyo na mwisho wake wanaacha fani kabisa.Alifafanuwa kuwa kuigiza ni zaidi ya urembo hivyo yeyote ambaye anafikiri anaweza kufanya kazi hii kwa uzuri wa sura na umbo ajaribu kama hakuchemka.

UREMBO SIYO KIPAJI NA SI KILA MWANAMKE MZURI ANAWEZA KUIGIZA

Muigizaji Jacqueline “Jackie” Wolper amewashangaa wanaodhani kuwa urembo wa mwanamke ni mbadala wa kipaji hasa katika sanaa ya maigizo.Al... [Read More]

Halima Yahaya ‘Davina’ mwanadada mwigizaji wa filamu hivi karibuni kajifungua mtoto wa kiume katika Hospitali ya Aga Khan na kumshukuru Mungu kwa kumwezesha kuzaa salama msanii huyo ambaye ni mahiri katika tasmia ya filamu alikuwa mwenye furaha wakati alipotembelewa na wa wasanii wenzake kwa ajili ya kumjulia hali na kumpa hongera kwa kujifungua salama.
Mwenyezimungu kwa kujifungua salama na nimepata Baby boy nimefurahi sana unajua siku mambo ya uzazi yanavyokuwa lakini pia asante kwa nyinyi rafiki zangu kuja kunitembelea na kujua hali yangu na mimi nipo salama kabisa na mtoto yupo sawa,”anasema Davina.Davina alitembelewa na wasanii wenzake katika Hospitali ya Agakhan kumpongeza wasanii hao walikuwa ni Jenifer Kyaka ‘Odama’, Salama Salmin ‘Sandra’, na kiongozi wa kundi la Bongo movie Herith Chumila wakiwa wenye furaha kwa rafiki yao kujifungua salama na kuwaletea mtoto wa kiume.

DAVINA AJIFUNGUA MTOTO WA KIUME

Halima Yahaya ‘Davina’ mwanadada mwigizaji wa filamu hivi karibuni kajifungua mtoto wa kiume katika Hospitali ya Aga Khan na kumshukuru M... [Read More]

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, TAFF, linawapongeza Waandishi wote kwa jitihada na ushirikiano mkubwa mnaouonesha kwa TAFF katika kuripoti shughuli na matukio yanayohusu tasnia ya Filamu nchini na Shirikisho kwa uwazi na weledi mkubwa katika kuihabarisha jamii ya Watanzania mambo mbalimbali yanayohusu tasnia na Wasanii kwa ujumla. Ndugu Waandishi ikumbukwe kuwa mnamo mwanzoni mwa mwezi Septemba 2011 Shirikisho la filamu Tanzania lilipokea rasmi taarifa za ugonjwa wa Msanii ambaye pia ni Muongozaji katika kampuni ya Wajey Film Saidi Jumaa Kilowoko aliyejulikana zaidi kwa jina la Sajuki.

Ndugu Waandishi kwa mujibu wa taarifa za kidaktari Sajuki alitakiwa kupelekwa nchini India kwa matibabu zaidi, katika kufanikisha matibabu hayo nchini India, Shirikisho la Filamu Tanzania ikishirikiana na Wadau mbalimbali wa Sanaa hapa nchini, Viongozi mbalimbali wa vyama na Serilaki, Wafanyibiashara kutoka kada tofauti za biashara kwa pamoja katika namna tofauti waliweza kuchangia gharama za safari hiyo,ambapo zaidi ya Tshs 32 milioni zilipatikana.
           
Hali ya Sajuki ilirejea katika matumaini baada ya kurudi India ingawa alitakiwa kurudi tena baada ya miezi mitatu kwa ajili kukamilisha tiba ,Tukiwa katika maandalizi ya kumrudisha India kwa matibabu, mwezi Disemba 2012 hali ya SAJUKI ilibadilika ghafla ambapo alipelekwa Hosptali ya Taifa Muhimbili na ikagundulika kuwa na upungufu mkubwa wa Damu na kansa ya ngozi. Wasanii na wadau mbalimbali waliitikia wito wa kuchangia damu na ilipatikana kama ilivyohitajiwa.

Ndugu Waandishi Wahenga walinena kwamba jitihada haziishindi kudra ya Mwenyeezi Mungu mpaka 02 Januari 2013 Saidi Juma Kilowoko alifariki dunia.

Kifo cha marehemu Sajuki kilivuta hisia za Watanzania wengi hasa kutokana na historia ya maradhi kwa muda mrefu, aidha Shirikisho la Filamu Tanzania,TAFF,linawashukuru Watanzania wote ambao waliweza kushiriki kwa hali na mali wakati wa kipindi chote cha maradhi mpaka umauti, hatuwezi kumkumbuka kila mmoja kwa nafasi yake.

Pamoja na hayo shukrani zimuendee Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Mrisho Jakaya Kikwete kwa kufuatilia kwa ukaribu maendeleo ya afya yake mpaka siku ya mazishi, pia tunawashukuru Viongozi wa Shirikisho la Muziki, Shirikisho la Sanaa za Ufundi, Viongozi wa vyama vya Siasa, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa vyama vya Wasanii,vyombo vya habari, ndugu na jamaa wa familia ya marehemu kwa ushirikiano waliouonesha kwa marehemu SAJUKI.

Tunajua hatuna cha kuwalipa lakini tunathamini michango yenu katika kumuuguza na mpaka siku ya kifo chake.Shirikisho la Filamu Tanzania tunaomba jamii ya Watanzania kuendelea kushirikiana na Wasanii katika Nyanja tofauti, lakini pia tunaomba vyombo vya habari viendelee kutoa habari zinazohusu tasnia ya filamu ambazo zitaonya, kuelimisha na kukumbusha wajibu wa Wasanii katika jamii kwa maendeleo ya Taifa letu.

Tunaomba Mwenyeezi Mungu awafariji na kuwapa moyo wa subira Wastara, Wazazi, ndugu na jamaa zake katika kipindi hiki kigumu na majonzi.Hatuna cha kufanya zaidi kwa marehemu Sajuki ila ni kumuombea dua kila tunapomkumbuka.

Tunamuomba Mwenyeezi Mungu aiweke roho yake mahala pema peponi

SHIRIKISHO LA FILAMU NCHINI "TAFF" YAWASHURU WAADHISHI WA HABARI

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, TAFF, linawapongeza Waandishi wote kwa jitihada na ushirikiano mkubwa mnaouonesha kwa TAFF katika ... [Read More]

Nyota wa filamu   Jaqueline Wolper kupitia kampuni ya JB Production ameingia ulingoni kwa ajili ya kuandaa filamu zake mwenye sambamba na meneja wake Leah Mwendamseke almaarufu kwa jina la Lamata, kwa kuanza kampuni hiyo tayari imekamilisha kurekodi filamu yao ya Malipo,

Lamata amesema filamu ya Malipo ni Hatari...Jack mwenye anasema mara nyingi anapopanga kufanya jambo lazima alimalize kwa asilimi mia kwa hiyo ameingia mzigoni na watu wategemee kuona maajabu kutoka katika kampuni hiyo ya kisasa zaidi na iliyojipanga kufanya kazi bora na zinazoelimisha.“Nimeingia katika fani ya utayarishaji na kwa kuanza ninakuja na filamu ya Malipo, ni filamu ya kipekee kuanzia hadithi, waigizaji wake wameigiza katika kiwango kikubwa cha kimataifa , ok si semi mengi bali mtaona katika filamu ya Malipo,Katika filamu ya Malipo wameshiriki wasanii wakali na Nyota kama Jaqueline Wolper, Blandina Chagula ‘Johari’, Stanley Msungu ‘Seneta’, Hashim Kambi ‘Ramsey’, Fatuma Makongoro ‘Bi. Mwenda’, Mgata, Ahmed Ulotu ‘Mzee Chilo, Slim na wasanii wengine kibao, filamu imeongozwa na Laeh R. Mwendamseke ‘Lamata’

WOLPER KUJA KIVINGINE NA MALIPO

Nyota wa filamu   Jaqueline Wolper kupitia kampuni ya JB Production ameingia ulingoni kwa ajili ya kuandaa filamu zake mwenye sambamba na... [Read More]

Wachezaji filamu maarufu Brad Pitty 48 na mchumba wake ambaye pia ni mcheza filamu wa Marekani Angelina Jolie 37 maarufu kama ‘Brangelina’ wameweka oda ya pete za dola mbili zenye thamani ya euro 500,000,kila moja kutoka kwa sonara maarufu Chanzo cha habri kilisema wako bize kutengeneza pete hizo za dhahabu na Almas zitakazofanana kwa wanandoa hawo watarajiwa,chanzo hicho kilibainisha kwamba Brad Pitt wiki iliyopita alimnunulia Angelina Jolie saa yenye thamani ya Euro 250,000 ambayo ni moja ya saa ya gharama duniani kama zawadi ya mpenzi wake kabla ya harusi yao ambayo itafungwa hivi karibuni ,wachumba hao wanawatoto sita kwa kipindi cha mahusiano yao kati ya watoto hao watatu ni wa kwao na wengine wamewaasili

BRAD PITT NA ANGELINA JOLIE KUCHONGA PETE EURO MIL 1

Wachezaji filamu maarufu Brad Pitty 48 na mchumba wake ambaye pia ni mcheza filamu wa Marekani Angelina Jolie 37 maarufu kama ‘Brangelina... [Read More]

Mcheza filamu Jennifer Aniston ambaye ni kati ya wasanii na muongozaji wa bora wa Filamu Duniani,ambaye alizaliwa Februari 11,1969,anakadiriwa kuwa na utajiri wa kiasi cha Dolla Million 115 sawa na shilingi Billioni 179 za Kitanzania..Utajiri huo ameupata kutokana na filamu alichocheza,alizoongoza na Matangazo ya Biashara ambayo ameyafanya..Aniston Pia anamiliki Jumba la kifahari linalokadiriwa kuwa na thamani ya dola 21Million,sawa na shilingi 32.7 Billioni za Kitanzania..filamu zilizo mpatia umaharufu mkubwa ni kama She's The One,Office Space,The Good Girl,Friends with Money na zingine ni kama Wanderlust, Horrible Bosses, Just Go With It, The Bounty Hunter, The Switch...na tayari alishawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Brand Pitt ambapo walioana Julai 29 ,2000 ambapo walitengana Januari 6,2005,Pia alishawahi kuwa na mahusiano na Vince Vaughn ambaye pia aliwahi kucheza nae filamu iliyokuwa ikijulikana kama The Break-Up.Hata hivyo waliachana nae akaingia katika mahusiano na Paul Sculfor na baadae na John Mayer na kwa hivi sasa yuko katika mahusiano na Justin Theroux ambao kwa pamoja wanaishi huko Los Angeles...

JENNIFER ANISTON ANA UTAJIRI ZAIDI YA $ 115 MILLIONI

Mcheza filamu Jennifer Aniston ambaye ni kati ya wasanii na muongozaji wa bora wa Filamu Duniani,ambaye alizaliwa Februari 11,1969,anaka... [Read More]

Wasanii  na wadau wengine waingia Mtaani na kukamata Dvd Feki kibao Maharamia wapatikana jirani kabisa na Maduka yanayouza kazi halali, Naibu Waziri Makala asikitishwa na wizi huo wa kazi za wasanii hapa nchini .. wimbi la wizi wa kazi za wasanii wa filamu  limeshamili zaidi na kukua kila kukicha Kampuni ya Steps Entertainment kwa kushirikiana na wadau wa filamu kuendesha msako kwa maharamia wanaojinufaisha kwa kazi za wasanii bila idhini ya wenye mali, mwizi wa kwanza alikamatwa siku ya Jumanne asubuhi baada ya mtego uliowekwa kumnasa Haramia mkubwa maeneo ya Kariakoo.asubuhi katika maeneo ya mtaa wa Magila na Likoma HaramiaBaadi ya wasanii walisikika wakisema “Hawajui shida tunazopata huko location kila siku tunagombana na
wasambazaji wakidai filamu zetu haziuzi lakini mtaani tunaziona kwa wingi, tunaumiza vichwa kumbe mwizi mwenyewe yupo jirani hata hatua kumi hazifiki, ninaumia sana maisha ninayoishi kwa kufanya kazi ngumu kisha kuna wanyonyaji wanakula bila kutoka jasho, watu kama hawa ni kuwafunga maisha,”Aidha nae  Rais wa Shirikisho la filamu ameeleza kuwa kampeni za kamatakama zimeanza baada ya kupewa idhini na Mh. Amos Makala Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Michezo na Vijana

OPARESHENI KAMATA MAHARAMIA WA KAZI ZA WASANII YAANZA KWA MAFANIKIO.

Wasanii  na wadau wengine waingia Mtaani na kukamata Dvd Feki kibao Maharamia wapatikana jirani kabisa na Maduka yanayouza kazi halali, ... [Read More]

MWIGIZAJI na mwandishi wa Muswada katika tasnia ya filamu  Susan Lewis ‘Natasha’ amesema kuwa pamoja na kuwa ni mkongwe katika tasnia hiyo ya filamu sekta hiyo bado haitegemei kwa sababu hailipi jambo ambalo linamfanya ajikute akiwa makini na biashara yake ya ubunifu na ushonaji wa mavazi, kazi inayomlipa kuliko hata filamu. “Tasnia ya filamu hailipi kabisa, kuna wakati ambao unaona kabisa jinsi ukipoteza muda wako katika kuhangaika na jambo lisilo lipa wakati kwa wenzetu ni ajira rasmi, unatumia nguvu kubwa lakini linavyokuja suala la malipo au kuuza filamu husika unababaishwa na wanunuzi jambo linatengeneza mazingira ya wasanii kujikuta wakidhulumiana kutokana na mazingira yaliyopo,”anasema.

Natasha anasema kuwa anatumia muda mwingi katika kuchagua filamu za kushiriki ikiwa katika kuwaunga mkono wasanii wachanga lakini si katika kutengeneza fedha, huku akisema kuwa mara nyingi katika tasnia ya filamu kumekuwa na taarifa zisozo sahihi kutoka kwa baadhi ya wasanii ambao wamekuwa wakijinadi kuwa wanalipwa fedha nyingi kwa kushiriki filamu hizo.“Kuna wakati ambao baadhi ya wasanii wamekuwa wakidanya kama wanalipwa fedha kuanzia milioni kwenda mbele jambo hili si kweli, mfano filamu inawashiriki zaidi ya 20 kila msanii akilipwa milioni tu, ukichanganya na gharama za uandaaji filamu hiyo gharama zake zinaweza kufikia hata milioni 25, je ni filamu ngapi ambazo zinauzwa zaidi ya milioni 35? Hapo ndio utabaini ukweli,”anasema Natasha.

FILAMU HAZILIPI

MWIGIZAJI na mwandishi wa Muswada katika tasnia ya filamu  Susan Lewis ‘Natasha’ amesema kuwa pamoja na kuwa ni mkongwe katika tasnia hiy... [Read More]

Msanii Issa Mussa ‘Cloud 112’ amesema kuwa watayarishaji wa filamu wamejikuta wakiwa katika wakati mgumu katika uandaaji wa filamu pale unapopewa bajeti kutoka kwa mwezeshaji na kuingia katika utendaji na kujikuta gharama zimeongezeka huku fedha iliyotolewa ikiwa chini.changamoto kubwa sana kuendelea au kusonga mbele katika tasnia ya filamu kwa huu mwendo tunaoenda nao kwa sasa, kwetu bajeti imekuwa ni tatizo tena tatizo kubwa, maisha yamepanda lakini kuna changamoto nyingi unakuta unapewa bajeti zinazofanana kwa kila filamu huku msambazaji akisahau kuwa filamu iliyopita inatofautiana na filamu mpya inayotengenezwa,”Hali hiyo inachangia filamu nyingi kuendelea kufanana au kuendelea kuonekana zikiwa zimetawaliwa vipande vya ndani ya nyumba Bar, au maeneo yanayojirudia rudia kwa kila filamu kutokana na ubanaji wa bajeti..

BAJETI NDOGO KATIKA FILAMU KIKWAZO KATIKA UBORA

Msanii Issa Mussa ‘Cloud 112’ amesema kuwa watayarishaji wa filamu wamejikuta wakiwa katika wakati mgumu katika uandaaji wa filamu pale u... [Read More]

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging