Mwigizaji wa filamu Bongo Emmanuel Myamba ‘Pastor Myamba’ wiki iliyopita aliagana na ukapera na kuamua kuwa mume wa mke halali Praxceda Kassela.
Harusi ya nyota huyo na mkewe mpendwa ilifungwa katika kanisa la
The River of Haeling Ministry of Tanzania na baadae katika ukumbi wa kisasa wa Zanzibar Beach Resort na kuhudhuriwa na watu mashuhuri na viongozi mbalimbali,
“Namshukru Mungu kwa Baraka zake kwangu na kwa mke wangu kwani ametuwezesha kufikia ndoto zetu yapaswa kufurahi sana na kupokea Baraka hizi, ni hatua vijana wengi wahitaji kuifikia asante Yesu,”anasema Pastor Myamba.