MWIGIZAJI wa filamu ya Mateso Ughaibuni Riyama Ali amefunguka kwa kusema kuwa filamu hiyo inatarajia kuzinduliwa Bongo mwishoni mwa mwezi wa tisa, filamu hiyo ambayo imewashirikisha wasanii kutoka Afrika Mashariki na Uingereza imekamilika.Filamu ya Mateso Yangu Ughaibuni tutaizindulia Tanzania kwa sababu pamoja kuwa imechezwa nchini Uingereza, na kutushirikisha wasanii nyota Tanzania, na imetumia Lugha ya Kiswahili, hivyo Tanzania inapewa heshima hiyo, “anasema Riyama Ali.
Sinema hiyo ya Mateso Ughaibuni imewashirikisha wasanii nyota kama kutoka Bongo ni Riyama Ali, Wastara Juma ‘Stara’, Khadija, na Issa Mussa ‘Cloud 112’ na wasanii wengine kutoka Uingereza, filamu hiyo inatarajiwa kuzinduliwa jiji Dar es Salaam mwezi Septemba.