Google PlusRSS FeedEmail

BALOZI DKT. BATILDA SALHA. BURIAN AOMBA FILAMU KUKUZA KISWAHILI

             
       Dr. Batilda Burian
BALOZI wa Tanzania nchini Kenya Mh. Dkt. Batilda Burian ameomba wasanifu wa Lugha ya Kiswahili kupitia Chawakama kusaidia watunzi wa filamu kutumia Lugha fasaha ya Kiswahili, kwa sababu Kiswahili ni bidhaa na Serikali ina mikakati ya kufundisha katika nchi nyingi.

“Tunaomba juhudi hizi za ukuzaji wa Lugha ya Kiswahili, muwasaidie wasanii wa filamu na muziki katika utunzi wao, watumie Lugha fasaha kwani wao ni rahisi kuwafikia watu kwa kutumia Filamu,”alisema Balozi Dkt. Burian.

         Dr. Batilda Burian
Chawakama wamepongezwa kwa juhudi zao za kukuza Kiswahili Afrika ya Mashariki na nje ya Jumuia hiyo, Balozi Dkt. Batilda amesema Tanzania ina mpango kufungua vituo vya kufundishia Kiswahili katika nchi za Afrika ya Kusini, Rwanda, Burundi, Nambia na nchi nyingine.

Zaidi ya watu milioni 90 inasemekana hujifundisha Lugha ya Kiswahili kwa kutumia filamu za Kitanzania ikiwa kama ni njia rahisi kwao kujifunza Kiswahili, nchi nyingi za Scandinavia hutumia njia hiyo, ni fursa nyingine kwa watengenezaji wa filamu Swahilihood kuitumia.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging