“Nilirudi Mtwara kwa ajili ya kufanya mtihani wangu wa darasa la saba, na nimerudi Dar tena kwa ajili ya kurekodi filamu ya Tmt Movie, siwezi tena kurudi Mtwara nitasoma hapahapa tu,”anasema Mwanaafa.
Mwanaafa anasema kuwa kampuni ya Proin Promotions imemjengea mazingira mazuri ya kuishi kama nyota hivyo hata kama anapasi mtihani wake atahamia hapa kwani kazi ya kurekodi filamu ambayo ndio kazi anayoamini si rahisi kuifanya Mtwara, filamu ya Tmt movie imeanza kurekodiwa na kinara ni Mwanaafa.