MWANA FA AMSHIRIKISHA ALIKIBA, KUACHIA NGOMA YAO JUMA TANO
Member wa zamani wa East Coast Team, Mwana FA anatarajia kuachia ngoma mpya Jumatano hii aliyomshirikisha Ali Kiba.
Mwana FA amemshirikisha Ali Kiba kwenye wimbo alioupa jina la ‘Kiboko Yangu’ alioufanya katika studio za MJ.
Mwaka jana Ali Kiba alipiga story na tovuti ya Times Fm muda mfupi baada ya kupost kwenye mitandao ya kijamii akiwa na Mwana FA ndani ya studio hizo na kueleza kuwa itakuwa surprise ya nguvu kwa mashabiki wao.
‘Kiboko Yangu’ ni wimbo ambao ulitarajiwa kutoka kabla ya ‘Mfalme’.