Google PlusRSS FeedEmail

ROSE AUMIA KUANDIKWA AMEBAKWA

Msanii wa filamu nchini Rose Ndauka ameweka wazi kuwa kitendo kilichowahi kumsikitisha katika maisha yake ni kuandikwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari jambo ambalo halina uwakika na halijathibitishwa na yeye mwenyewe.

Ambapo aliweka wazi kuwa jambo ambalo limemuumiza na hatolisahau ni kuandikwa na moja ya gazeti hapa nchini jambo ambalo kwake anaona si la kawaida.

"Nimeandikwa nimekunywa nimelewa kisha nikabakwa na wanaume zaidi ya watatu, jambo hilo liliniumiza sana na ni jambo ambalo sitoweza kulisahau katika maisha yangu kwani ni kitu ambacho nakikumbuka kila siku" alisema Rose.

Aliongezea kuwa ni vyema waandishi wakatafuta story za ukweli na kuwauliza wausika.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging