MAZISHI ya msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Geez Mabovu ambaye alikuwa maarufu kwenye muziki wa Hiphop Tanzania, yamefanyika jana nyumbani kwao Iringa katika makaburi ya Mlolo.
Mabovu amefariki dunia kwenye hospitali
alikokua amelazwa nyumbani kwao Iringa alikokwenda wiki mbili zilizopita
kutokea Dar es salaam akisumbuliwa na maradhi ya kifua.
Ndugu, jamaa, marafiki, wasanii na watu mbalimbali wamejitokeza kushiriki katika mazishi hayo.