Google PlusRSS FeedEmail

REY'AWAASA WASANII WANAOCHIPUKIA"


Muongozaji na mwigizaji nyota wa filamu Bongo Vincent Kigosi ‘Ray’ amewaasa wasanii wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamu kuwa wasitukane wakongwe waliopigania tasnia hiyo, leo tasnia inatolewa macho na kila mtu na kutoa ajira kwa watu mbalimbali hata Serikali imeliona hilo.

“Tasnia hii watu waliisusia ilikuwa ikionekana kama ni kazi ya ziada tu wala si kazi inayomwezesha mtu kuendesha maishayake, katika hali ngumu tulipigana na kufikia hapo ilipo ni kwa juhudi za wasanii pekee hawa ambao leo unaweza kuwabeza kwa sababu tu upo nao nawe unauza filamu zako,”anasema Ray.

Ray anasema kuwa katika kuhakikisha kazi zinakuwa bora kila mara utumia muda mwingi katika kuongeza vifaaa vya kisasa sambamba na kutumia watu wenye ujuzi wa filamu, lakini bado anajua kuwa kuna watu ambao akiwa nao ujifanya kumsifia akiwapa kisogo tu umponda, anashauri vijana washindane katika kazi na sikupoteza muda kwa kuwabeza watu.

“Huwezi kumdharau mtu kama Ally Yakuti kwa kusema eti kazeeka kiuandishi, ni dharau na kusahau mchango wa watu walioifikisha tasnia ya filamu hapa ilipo bila kuwepo hao tusingefika hapa tulipo,”anasema Ray.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging