Proin Promotions imeamua kutoa support kwa watayarishaji na wasambazaji wadogo wadogo kuwazalishia sinema kwa bei ya chini kabisa katika ubora wa hali ya juu, kampuni inawakaribisha wote wale ambao wana nia ya kutengeneza filamu zao na kusambaza wenyewe badala ya kutegemea makampuni makubwa.
Proin imeamua kuchukua jukumu hilo baada ya kugundua kuwa kuna watayarishaji wana uwezo wa kusambaza kazi zao lakini wanakwama katika suala la kurudufu na kuzalisha nakala za kutosha, hali inayofanya kazi nyingi kuingia katika foleni kwa kuzitegemea kampuni za usambazaji.
Kwa sasa unaweza kupata nakala moja kwa bei ya Tshs. 650 hadi Tshs. 800 kwa mtayarishaji yoyote anakaribishwa kutumia fursa hiyo adimu kutokea katika kukuza tasnia ya filamu Swahilihood filamu katika ofisini za Proin Promotions zilizopo Mikocheni.