“Hayo tunayoona wasanii kutengana soko la filamu zetu kushuka viwango ni laana ya Kanumba kwa tunayomtendea, Kanumba alipigania sanaa kimataifa na leo tunaona kazi zake pamoja amefariki lakini watu wa mataifa wanaona umhimu wa Kanumba lakini sisi tumebaki na chuki zetu,”anasema Steve.
“Nasema tena filamu zetu kuuzwa buku Jero ni laana ya Kanumba, unafiki kutopendana ni Laana ya Adam Kuambiana, tumewaacha wenzetu waliotutangulia bila chochote,”
Msanii huyo alizidi kulalamika kuwa kuna watu waliwahi kusema kuwa yeye alikuwa chanzo cha ugomvi wa marehemu na kundi la Bongo movie lakini yeye ndio kafika katika uzinduzi lakini wale waliojifanya wema hakuna hata mmoja aliyefika katika uzinduzi wa kitabu cha The Great Fallen Tree uliofanyika katika ukumbi wa Landmark Hotel.