Google PlusRSS FeedEmail

MAMA KANUMBA AKUMBANA NA CHANGAMOTO ZA UMAARUFU

                             



Flora Mtegoa mama mzazi wa msanii nyota marehemu Kanumba ameanza kuonja adha ya umaarufu na kukiri kuwa kuwa kumbe mwanaye alikuwa ana kazi kubwa kwa wanajamii kutokana na umaarufu aliokuwa nao, kwani hali hiyo imeanza kumtesa baada ya kushiriki katika filamu kadhaa.

            

“Mwanangu nakwambia umaarufu ni shida kubwa, zamani nikirudi nyumbani Bukoba nilikuwa nina amani kwani hakuna hata aliyeniona kama ni mtu maarufu, lakini baada ya kifo cha Kanumba na mimi kuingia kuigiza na watu kunijua ni shida,”anasema Mama Kanumba.

Mama Kanumba anasema kuwa hivi karibuni alifiwa na kwenda msibani Bukoba, alijikuta katika wakati mgumu kwani kila kitu alikuwa akisakiziwa yeye kwa sababu tu ameonekana katika filamu na wanaamini kuwa anapesa nyingi, hivyo inapofikia suala kutoa fedha au kununua chochote anaangaliwa yeye...

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging