Google PlusRSS FeedEmail

NYOTA MBOFU AZUNGUMZIA CHANGAMOTO ALIZOKUTANA NAZO KWENYE VITUKO SHOW

                   Griady Kahena
MCHEKESHAJI na muigizaji wa filamu Bongo Griady Kahena ‘Nyotambofu’ amefunguka sababu ya kumfanya iliyomfanya apumzike kuigiza katika kundi la vituko show kipindi kionyeshwacho Channel Ten sababu ilikuwa ni bosi wake kutowajali wasanii hasa wakiwa na shida.

Sasa hivi hakuna kitu kabisa ukiangalia Vituko show kama tulivyokuwa sisi magwiji tulianza na kundi hilo, wengi tumekimbia baada ya kuona bosi haoni umuhimu wetu pamoja na kufanya kazi lakini msanii maarufu huna pesa, huna shida unazimiwa simu,”anasema Nyotambofu.

Nyota mbofu ambaye kwa sasa ni mtangazaji katika kipindi cha MinBazz kirukacho katika Televisheni ya Star tv, msanii amebainisha kuwa kufuatia utaratibu wa bosi wao kuwachukulia kama wasanii wa kawaida tu wengi wamejitoa na kuangalia kazi nyingine badala ya kuigiza.

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging