Imenishtua sana maana asubuhi ya jana nimekuta kwenye gazeti wameandika nikashangaa yaani hapa nimekaa kwa sababu muda mwingi siendeshi mimi akaunti yangu ya twitter,anaiendesha mtu wangu wa blog Bestizo maana nilikua nataka kutoa tamko’
‘Hakuna kitu ambacho namdai Diamond,hakuna siku hata moja nimefikiria kwenda kumshtaki Diamond labda kama kungekua kuna kitu chochote,yaani labda kungekua na ukweli wa kitu chochote siwezi kupoteza muda wangu kwenda polisi,sijawahi kufanya kitu cha namna hii hizi taarifa zimenishtua sana’
‘Sijawahi kujiunga Vikoba maana sivijui,nilikua nimekaa na mtu akanambia labda Wema hujui hawa watu wa vikoba kwanza mimi siwezi kukopa Milioni 10.