STAA mwenye nyota Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kwa kubainisha wazi kuwa wasanii wa filamu wa kike kama wana mafanikio yao yanayoonekana hayatokani na malipo ya sinema wanazoigiza bali wanabiashara nyingine zilizojificha ndani yake na si fedha za filamu.
“Wengi wanaamini kuwa wasichana wa Bongo movie filamu zinawalipa sana na kuwa watu wenye fedha lakini hali ni tofauti sana na mawazo ya wengi, na hii inatokana na uwezo wetu wa kuwaza na kufanya makubwa tulipo tumedumaa lakini hakuna anayeona,” anasema Lulu.
Lulu amedai kuwa hakuna msanii anayewaza mawazo makubwa zaidi ya kufikiri kuhusu kuvaa, hakuna mtu anafikiria kuigiza na wasanii wa kimataifa kama Ritha Dominic ili sanaa imlipe na sikutegemea mapedje au biashara zisizo rasmi, kwani filamu inaoneka ipo juu lakini wahusika wake haiwalipi kwa staili nyingine.