“Soko letu linabana sana kama hauna shughuli nyingine kichwa kinawaka moto, nimetoa filamu yangu ya Msala nimewapa zawadi watanzania nataka ifike popote ndio maana nimwapa hawa jamaa wasambaze nimerudisha mpira kwa kipa,”anasema Ritchie
Ritchie anasema kuwa filamu yake ya Msala inafungua mwaka angependa kila mtu aipate lakini anasema hali ya soko itaendelea katika hali kama hii basi ataacha na uigizaji na kuingia katika kilimo rasmi yupo katika maandalizi ya kuwa mfugaji na mkulima lakini sio kama anaacha kuigiza.