Uhusiano kati ya mastaa hao wawili uliingia dosari siku ya fainali ya shindano la Big Brother Africa ambapo baada ya Idris kushinda Davido alitweet ‘And They Cheat Again’ na Diamond ambaye usiku huo alishinda tuzo ya TFA za Nigeria aliijibu kwa ujumbe wa kuibeza.
Kufuatia tweet hiyo ya Davido, watanzania wengi walimshambulia kwa matusi na kumtaka aombe radhi kitu ambacho aligoma kufanya.
Tangu hapo, kumekuwepo na maneno kuwa uhusiano kati ya wawili hao umevunjika na ndio maana imekuwa rahisi kwa wengi kuhusu tweet hizo zilizokuwa zikimlenga Diamond.