Nova amedai kuwa tatizo lilikuwa ni kodi kwani kodi imekuwa ikipanda kila mwaka hivyo walimudu kulipa kwa miaka miwili kwa pamoja wakaona haina sababu kulipa kodi kubwa bila sababu ya msingi waktai wanaweza kufanya kazi popote.
Hivi karibuni kuna minong’ono ambayo imekuwa ikisikika kuwa moja ya sababu ya kampuni hiyo kudorora ni mama mzazi wa marehemu kuingilia kufanya kazi ambazo hana ujuzi nazo, jambo ambalo limewafanya wasaidizi wake wakimbie na kuiacha kampuni hiyo ifie mikononi mwake.