Google PlusRSS FeedEmail

UTAFITI:WANAUME WANAPENDA WANAWAKE WENYE MAKALIO MAKUBWA


Je wajua kwanini wanaume wanawapenda wanawake waliojaliwa na makalio makubwa ?

Katika majarida mengi umewaona wanaume wakikodolea macho picha za wanawake wenye makalio makubwa iwe ni kim Kardashian, Jenipher Lopez Nicki Minaj na Vera Sidika kutoka Kenya .

Sasa basi Utafiti umedhibitisha kuwa ni kweli wanaume wanapenda wanawake waliojaaliwa sehemu ya nyuma.

Kulingana na utafiti wa chuo kikuu Bilkent , chuo kikuu cha Texas, na chuo kikuu cha American University kilichoko mjini Beirut

Wanaume wanakisia kuwa mwanamke mwenye makalio makubwa anaweza kufanya kazi kwa bidii zaidi ya mwanamke ambaye hana makalio makubwa.

Hata hivyo kinachowavutia wanaume si makalio haswa bali ni kupinda kwa uti wa mgongo unaosababisha tako kuonekana zaidi.




Utafiti huo unasema kuwa upinde wa 45.5 ndio unaovutia wanaume zaidi.

Wanaume walioneshwa picha za makalio ya wanawake wengi na asilimia kubwa iliwapendelea wanawake wenye makalio yaliyopinda kwa kiwango cha 45.5

Aidha zaidi ya asilimia 30% walisema wangalimchukua mwanamke mwenye makalio makubwa zaidi ya yule waliye naye sasa.

Kwa mujibu wa utafiti huo katika miaka ya awali mwanamke aliyeonekana kuwa na makalio makubwa alipendelewa kutokana na uwezo wake wa kubeba mizigo mgongoni.

Isitoshe mwanamke kama huyo aliwavutia wanaume wengi na hivyo kuwa na uwezo wa kuzaa watoto wengi.

Aidha mwanamke mwenye makalio makubwa angeweza kustahili uzito wa mtoto aliyebebwa tumboni na hata kustahilimi makali ya uzazi kuliko wale wenye makalio wastani.


HISANI YA BBC

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging