Google PlusRSS FeedEmail

JUSTINE BIEBER AVUNJA PENZI LA BIG SEAN



Imeripotiwa Big Sean na Ariana Grande wameachana na kila mtu kushika njia yake. Hii inatokea sikuchache baada ya diss ya mameno ya mitandaoni kutoka kwa Big Sean kwenda kwa Justine Biber akimpiga mkwara mzito Bieber na kumwambia ajichunge na ajue namna ya kucheza na wapenzi wa watu akiwa jukwaani.

Wiki chache Ariana Grande na Justine Biber walipanda jukwaa moja na kufanya shoo na kufanya vituko vya kushikanashikana na kukumbatiana mara kwa mara vilimkera rapa Big Sean.

Hata hivyo Big Sean na Ariana Grande wamesema wenyewe wameamua kuachana kutokana na ratiba za shoo zao kubana hivyo na kuwatenganisha kwa muda mrefu na kutoona raha ya penzi, kwa hiyo ni bora wabaki tu kuwa marafiki wa karibu. Wawili hao wamedumu kwenye uhusiano kwa muda wa miezi nane tu na hii imekua ni kawauida kwa mastaaa kupigana chini baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa muda mfupi

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging