“Kinachotukutanisha pale ni kazi sasa mtu mwingine anavyoleta utoto na ni mtu mzima haipendezi, wanadharau sana hasa wakiitwa masupa star vichwa vinavimba sana, lakini bila nidhamu katika kazi ni sawa na bure, ndio maana hakuna msanii anayejiita star anafanya kazi na wazungu,”anasema Mbembe.
Msanii huyo amesema kuwa moja ya sifa kubwa ya msanii ni kujiheshimu pamoja na kuheshimu kazi unayotakiwa kufanya na si vinginevyo lakini si wasanii wenye majina wa kibongo ambao wanajua wajibu wao wakiwa kazini jambo ambalo linasababisha tasnia ya filamu kushindwa kusonga mbele kwa kukosekana nidhamu.