Actress grade one Bongo, Elizabeth ‘Lulu’ Michael amedai kati ya ‘couple’ anazozielewa Bongo ni mapenzi kati ya Mwanamuziki ‘Performer’ Shilole na mmiliki wa hit ‘Bilima Nuh Mziwanda.
Akizungumza kupitia kipindi cha ‘the playlist’ cha Times Fm, Lulu amedai kiukweli anawapenda sana na amejikuta akiwapenda siku hadi siku kwa vituko vyao.
“Nawapenda kwa kweli, nawapenda sana yani(akicheka), the way wanaishi tu na maisha yao wanavyoyaendesha yani” alisema Lulu.
Kauli hiyo ya ‘Lulu’ inakuja, ikiwa ni siku kadhaa baada ya Ney wa mitego kupost picha na maelezo iliyotafsiriwa na ‘followers’ wake zaidi ya laki 2 Instagram kama ‘dongo’ kwa Nuh. “Mtag mwanaume anayefugwa na mwanamke hapa” aliandika Ney