Taarifa mpya imeripotiwa kuwa rapper bilionea mmiliki wa Gambe ya Ciroc Diddy, amefutiwa mashitaka yake yote aliyokuwa akikabiliana nayo katika kesi ya kushambulia.
Pamoja na kufutiwa mashitaka hayo, Diddy atatakiwa kuripoti halmashauli ya jiji la Los Angels tarehe 15 mwezi wa 10.
Rapper huyo alitenda makosa hayo mwezi wa 6 mwaka huu, na alikuwa akituhumiwa kwa makosa 3 ambayo ni kushambulia kwa silaha, viashiria vya kigaidi na kuumiza.
Kingine ni kwamba mkali huyu atatakiwa kuhudhuria darasa la kukabiliana na hasira kwa siku 180.