OMARION NA MPENZI WAKE WATARAJIA MTOTO WA PILI
Maisha yanamuendea vizuri rapper Omarion siku hizi, ngoma yake ya ‘Post to be’ inapata ‘Rotation’ ya kutosha kwenye Radio na TV nyingi duniani, mkali huyo wa MMG kwa sasa yeye na mpenzi wake wanajiandaa kumkaribisha mtoto wa pili kwenye familia yao.
Omarion amesanua hilo kupitia Instagram, akiweka michoro ya kitaalam inayoonyesha kiumbe kidogo kikiwa tumboni akiipa ‘Caption’ ya “Mrembo wangu yuko mbioni kufika”.
Wawili hao tayari wana mtoto mmoja anayejulikana kama, Megaa Omary Grandbury.