Google PlusRSS FeedEmail

FLORA AFUTA KESI DHINI YA MUMEWE

      

Ndoa ya Flora Mbasha na mume wake Emmanuel Mbasha bado ipo hai baada ya wawili hao kukubali kuifuta kesi ya talaka iliyodumu kwa takriban mwaka mmoja.

Flora ndiye aliyefungua kesi hiyo baada ya kutokea mgogoro kwenye ndoa yao iliyosababishwa na kesi ya kudaiwa kubaka aliyoshtakiwa mumewe. Hata hivyo Emmanuel hivi karibuni alikuwa mtu huru baada ya kushinda.

Mwanasheria wa Flora, Edo November amedai kuwa wawili hao wamekubaliana kuifuta kesi hiyo kwaajili ya uhai wa familia yao yenye watoto wawili.

“Ninachoweza kusema ni kuwa yule ni mume wangu bado ninampenda,”  “Tunamshukuru Mungu kwa hilo na kila mmoja amekuwa na amani ndani ya moyo wake,” aliongeza.

Mbasha alisema bado wana mpango wa kuikuza familia yao. Kuna tatizo moja lakini ili kufanikisha hili – Emmanuel Mbasha hayuko tayari kurudiana na mke wake!!

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging