Google PlusRSS FeedEmail

ALLY KIBA ATUA LOS ANGELES, KUIPIKA CHEKECHA CHEKETUA



MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ally Kiba afika jiji la Los Angeles nchini Marekani kwa ajili ya maandalizi ya video ya wimbo wake wa Chekecha cheketua, hali hiyo inapelekea Ally Kiba kuwa miongoni mwa wasanii wakubwa waliovuka hatua kufanya video nje ya nchi.

Chekecha Cheketua ni ngoma yake ya mwisho kutoa na kuonekana kuitendea haki .Ally Kiba hakuwa msanii wa kufanya video zaidi katika muziki, lakini sasa imekuwa tofauti katika muziki wake, hii ni kutokana na changamoto iliyokuwepo kwenye soko la muziki wa kizazi kipya.

Ally kiba ameamua kupaa zaidi baada ya kutua Marekani katika Jiji la Los Angeles kwenda kufanya video yake ya wimbo wake mpya.Hata hivyo Ally Kiba amekuwa tofauti zaidi baada ya kumtumia choreographer Aliya Janel ambaye amewahi kutokea kwenye video za wakali kama Nick Minaj na Chris Brown.

Kupitia mtandao wa Instagrama Ally Kiba alipost”In L.A And We Are Getting Ready For My Upcoming New Video . In The Makeup Room With My Leading Lady @aliya_janell #kingkiba
Baadhi ya picha katika mchakato huo ni hizi hapa chini

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging