Juma Kassim Kiroboto ‘Nature’ amefyatuliwa risasi katika tukio la ugomvi Mtu ambaye anadaiwa kumfyatulia Nature risasi hajafahamika lakini inadaiwa ni mtu wake wa karibu waliyetibuana katika mazingira ya ‘kula bata’.
Awali vyanzo vyetu vilidai kwamba wawili hao, walitibuana wakiwa kwenye klabu moja iliyopo Temeke, Dar es Salaam Alhamisi iliyopita.
Hata hivyo, chanzo kingine kilidai kwamba Nature alitibuana na jamaa yake huyo mtaani kwao Temeke.
“Jamaa alifyatua risasi lakini alipiga juu, hakumlenga Nature. Unajua ilikuwa ni ugomvi mkubwa, kwa hiyo Nature baada ya kusikia milio ya risasi alilala chini kwa sababu aliamini anampiga yeye,” kilisema chanzo chetu.
Awali vyanzo vyetu vilidai kwamba wawili hao, walitibuana wakiwa kwenye klabu moja iliyopo Temeke, Dar es Salaam Alhamisi iliyopita.
Hata hivyo, chanzo kingine kilidai kwamba Nature alitibuana na jamaa yake huyo mtaani kwao Temeke.
“Jamaa alifyatua risasi lakini alipiga juu, hakumlenga Nature. Unajua ilikuwa ni ugomvi mkubwa, kwa hiyo Nature baada ya kusikia milio ya risasi alilala chini kwa sababu aliamini anampiga yeye,” kilisema chanzo chetu.








