Google PlusRSS FeedEmail

MPELELEZI : WHITNEY HOUSTON ALISHAMBULIWA KABLA YA KIFO CHAKE




Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwenye mitandao zinaeleza kuwa mpelelezi huyo alisema taarifa za hospitali zilidai kuwa kifo chake kilitokana na kuzama kwenye maji wakati akioga na ugonjwa wa moyo baada ya kutumia dawa za kulevya kwa wingi

Alisema baada ya wataalamu kuufanyia uchunguzi mwili yake walidai kuwa walimkuta mfumo wake wa damu ukiwa na kiwango kikubwa cha dawa za kulevya aina ya cocaine lakini mwili wake haukuwa na jeraha lolote

Mpelelezi huyo alisema kuwa amefanya upelelezi na anao ushahidi unaonyesha kuwa nyota huyo aliuwawa na kifo chake hakikutokana na ajali ya kuzama katika maji baada ya kubwia dawa za kulevya

Mpelelezi huyo alikabidhi vielelezo vya ushahidi huo ambavyo vinaonyesha mwimbaji huyo aliuwawa kutokana na deni la fedha za dawa za kulevya zipatazo dola za Marekani milioni 1.5

Alisema ushahidi huo unaonyesha majeraha wakati nyota huyo akiwa anapambana na mashambulizi hivyo anaamini kuwa nyota huyo alishambuliwa na mtu waliyekuwa anamdai fedha hizo wakati akiwa katika hoteli hiyo

Haikuwa mara ya kwanza wafanyabiashara wa madawa ya kulevya kushambuliwa ili kulipa deni wanalodaiwa

:Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali ya kimataifa

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging